|

SHIRIKA LA VIWANGO TANZANIA (TBS) KWA UFUPI
Shirika la Viwango Tanzania (TBS) ni Shirika la
Umma chini ya Wizara ya Viwanda, Biashara na
Masoko, lililoundwa chini ya Sheria ya Bunge
Nambari 3 ya mwaka 1975 na kurekebishwa chini ya
Sheria Namba 1 ya mwaka 1977.
MAJUKUMU YA TBS
TBS ina majukumu makuu manne:
-
Kuweka na
kusimamia viwango vyote vya kitaifa.
-
Kutoa ushauri
viwandani juu ya uzalishaji wa bidhaa bora.
-
Kupima na
kuhakikisha vipimo vinavyotumika viwandani.
-
Kuelimisha
umma juu ya masuala yote yanayohusu uwekaji na
usimamiaji wa viwango pamoja na udhibiti wa ubora
wa bidhaa viwandani.
VIWANGO VYA TANZANIA
Viwango vya Tanzania ni viwango vya kitaifa
vilivyokwishawekwa au vitakavyowekwa kwa mujibu wa
Sheria ya Viwango Na. 3 ya mwaka 1975 vikielezea
kanuni za uzalishaji, uhifadhi na ufungashaji wa
bidhaa bora.
Mpaka sasa TBS imeishaandika viwango zaidi ya
1000
katika nyanja za Kilimo na Chakula, Ngozi,
Kondom, Madawa,
Nguo, Uhandisi mitambo, Uhandisi ujenzi na
Uhandisi umeme.
UTEKELEZAJI WA VIWANGO
Viwanda kadhaa hapa nchini, vya serikali pamoja na
vya watu binafsi, hufuata na kutumia viwango vya
kitaifa katika uzalishaji na uuzaji wa bidhaa
mbalimbali nchi za nje.
Ili wananchi waweze kufaidika na viwango, TBS
inaendesha mpango wa uthibiti wa ubora wa bidhaa,
ambao unaliwezesha Shirika kutoa leseni kwa
wazalishaji bidhaa wanaothibitishwa kuwa
wanazalisha kulingana na kiwango cha kitaifa cha
bidhaa husika ambayo huwaruhusu kutumia alama ya
‘’tbs’’ ya ubora wa bidhaa.
FAIDA ZA VIWANGO
-
Huweka usawa
katika uwanja wa biashara
-
Huondoa
mkanganyiko kuhusiana na bidhaa
-
Husaidia
kufungua masoko zaidi
-
Hurahisisha
biashara baina ya nchi na nchi
-
Hutoa
uhakikisho wa ubora, usalama, kuaminika na ufanisi
-
Huipa serikali
urahisi wa kuunda sheria zinazohusiana na masuala
ya afya, usalama na uhifadhi wa mazingira
-
Hulinda afya
na usalama wa walaji/watumiaji wa bidhaa
mbalimbali.
FAIDA ZA ALAMA YA UBORA
YA 'tbs'
Kwa mteja/mlaji
-
Humthibitishia
kuwa bidhaa husika inafaa kwa matumizi husika
-
Huwezesha
kupungua kwa bei ya bidhaa kutokana na ushindani
-
Humhakikishia
usalama wake kiafya na katika matumizi
-
Huongeza ubora
wa maisha
-
Hulinda
mazingira yake.
Kwa
mzalishaji
-
Humpa uwezo
mkubwa zaidi wa kushindana sokoni
-
Humpatia
wateja zaidi
-
Humwondolea
usumbufu wa kupima bidhaa kwa kuzingatia matakwa
ya mnunuzi
-
Humkinga dhidi
ya ushindani na bidhaa duni zisizo na viwango.
MAABARA
TBS ina maabara saba zenye vifaa vya
kisasa na wataalamu wa kutosha katika nyanja za
madawa, kilimo na chakula, nguo/kondom/ngozi, uhandisi
mitambo, uhandisi ujenzi, na uhandisi umeme pamoja
na maabara ya ugezi.
Kwa maelezo zaidi tuandikie kwa kutumia anwani hii:
Shirika la Viwango Tanzania
S L P 9524 Dar es Salaam
Tanzania
Simu: +255 22
2450206 / +255 22
2450949
Faksi:+255
22 2450959
Barua pepe:info@tbstz.org
Tovuti:
www.tbstz.org
Au tuone katika eneo la UBUNGO, Dar es Salaam
kwenye kona ya Barabara za Morogoro na Sam Nujoma.
(Read
more about TBS Services)
[Top]
|